Matthew 23:37-39

Yesu Aililia Yerusalemu

(Luka 13:34-35)

37 a “Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako pamoja, kama vile kuku akusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake, lakini hukutaka! 38 bTazama nyumba yenu imeachwa ukiwa. 39 cKwa maana nawaambia, hamtaniona tena tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana.’ ”

Copyright information for SwhNEN